Ads 468x60px

.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

FOLLOW US ON TWITTER

FOLLOW US ON TWITTER

.

Monday, August 27, 2012

Al-Shabaab Yaamua Kuuza Nyama Ya Fisi ili Kugharimia Operesheni Zao Za Kijeshi

Wafanya biashara wa al-Shabaab wanawaambia wakazi wa Kismayu kuwa kula nyama ya fisi itawalinda na maradhi na jicho la uovu. Juu, mwanamke anauza nyama huko Dinsor.
Al-Shabaab wameanza kuuza nyama ya fisi katika mji wa bandari kusini ya Somalia kama njia ya kukusanya pesa kwa ajili ya operesheni za kijeshi kabla ya kukaribia kwa vita dhidi majeshi ya Somalia na washirika wake , wachambuzi wasema.
Masheikh wa Somalia ambao kwa karne nyingi wamekuwa wakichukulia kuwa ulaji wa nyama ya fisi kulikatazwa na Uislamu kwa vile mnyama huyu hula miili ya maiti wa kibinadamu na wanyama.
Hatua hii mpya ni moja ya dalili nyingi za kuchanganyikiwa kifedha kwa washirika wa kikundi cha al-Qaida wakati majeshi ya Somalia na washirika wake yanaendelea kuziteka kambi za al-Shabaab nchini kote.
Ili kuwashawishi wakaazi kula nyama hiyo, ambayo mara nyingi ina magonywa kwa sababu mnyama huyo anakula mizoga, wafanya biashara wa al-Shabaab wamekuwa wakitumia uchawi wa asili ili kuwanasa wale wasiofahamu vyema, alisema Suleiman Abdi Guled, mpishi katika Hotel Alkhalej mjini Mogadishu ambaye ana familia huko Kismayo.
Kwa mujibu wa watu wanaofanya uchawi, nyama ya fisi ni nzuri kwa kujikinga na maapizo na dhidi ya magonjwa na jicho la ubaya.
"Ni ishara ya kutisha kwa sababu ni nje ya mila [za Kisomali] kula nyama ya fisi, hasa kwa vile wapo wanyama wengine wa kuliwa," alisema. "Al-Shabaab ni kikundi kilichopotea ambacho kinajaribu kutumia fisi na uchawi kwa operesheni zao za kijeshi."
Khalif Mohamud, mfanya biashara wa Kismayo, alisema al-Shabaab wanapata pesa katika biashara hii kwa kuudhibiti uchinjaji wa fisi.
"Al-Shabaab wanayo majumba ya machinjio mjini na tunalazimika kulipa pesa kwa kuchinja na kuchuna wanyama baada ya mawindo," aliiambia Sabahi.
Nyama ya fisi -- imeruhusiwa au kukatazwa kidini ?
Sheikh wa Somalia Sheikh Mohamud Awabdulle Ariif alisema watu wamekatazwa kuwinda na kula nyama ya fisi kwa mujibu wa sharia.
"Fisi ni miongoni mwa wanyama wadanganyifu na walafi, kwa vile wanawinda kondoo na kula nyama ya binadamu," alisema. "Pia hufukua makaburi na kutoa na kula maiti, pamoja na kula mizoga ya wanyama, wadudu na mabaki ya mawindo mengine."
Mursal Issac, mwanaharakati wa jumuiya ya kiraia mjini Mogadishu, alisema hali mbaya ya kifedha ya al-Shabaab imekipelekea kikundi kuamua kufanya biashara ya mkaa na nyama ya fisi ili kugharimia operesheni zake za kijeshi.
"Fisi ni wanyama wachafu wanaokula mizoga ya wafu, na ndio sababu ninawataka ndugu zetu wa Kismayo kujizuia na kula nyama yao," aliiambia Sabahi. "Tumebarikiwa na Mungu ardhi na wanyama wa baharini, na nadhani ni bora kujiweka mbali na mnyama huyu."
Issac alisema al-Shabaab inajaribu kunyanyua hali yake mbaya ya kifedha kwa sababu inaogopa kushindwa kijeshi mikononi mwa Jeshi la Somalia na Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM).
Sagal Hassan Ali, ambaye anafanya kazi katika mkahawa mdogo katika kiunga cha Via Afmadow, Kismayo, alisema yeye hatakula nyama ya fisi na hata asingewinda mnyama huyu muovu.
Aliiambia sabahi kuwa anachukizwa kuwa soko la hapo limegeuzwa uwanja wa kufanyia biashara ya nyama hii.

0 comments: