Msanii aliyefanya vizuri katika ngoma ya '' Chop my money'' aliyoshirikishwa na Psquare akiwa sambamba na Akon ,Mr. MayD baada la mgogoro kati yake na Psquare na kutolewa katika lebo ya ''square records'' inayomilikiwa na wasanii hao [psquare] ameamua kuanzisha lebo yake binafsi inayokwenda kwa jina la ''Confam Entertainment'' itakayo wahusisha wasanii hasa kutoka UK na itakua inahusika na muziki wa radha tofauti tofauti. Lengo la kuanzisha lebo hiyo inasemekana ni ushindani na Psquare kwani toka msanii huyo aondolewe kienyeji na Psquare records amekua akitafuta njia ya kujitangaza kivyake. kabla ya kufanya kazi zake lebo ya square records mr. may d alikua anafanya kazi zake katika lebo ya ''Ice cream records'' |
0 comments:
Post a Comment